Mapitio ya Premier Bet Tanzania 2024

Premier Bet

Tested & Verified on 20 April 2024
Last updated April 17, 2024

Kwenye mapitio  haya ya Premier Bet Tanzania, yatatolewa maelezo ya kina kuhusu huduma zinazopatikana kwenye jukwaa hili. Huduma zitolewazo ni machaguo yaliyopo kubashiri matokeo ya michezo, tovuti za kasino na codes za Premier Bet. Endelea kusoma ili kufahamu kwa undani zaidi kupitia mapitio ya Premier Bet.  

Kuhusu Premier Bet Tanzania

Tangu kuzinduliwa kwake mwaka 2016, Premier Bet imekuwa ni jukwaa la michezo ya kubahatisha lenye makazi yake Afrika ambalo linakuwa kwa kasi. Hadi sasa, kampuni inaendesha shughuli zake kwenye nchi mbalimbali karibu  20.

Aidha, Premier Bet Tanzania ni kampuni inayoendesha michezo ya kubahatisha na michezo ya kasino kwa wanaobeti nchini. Kampuni inatoa huduma za kubeti kupitia odds za michezo ya aina mbalimbali na matukio mbalimbali ya kimichezo, promosheni, na uwekaji dau wakati mchezo umeshaanza. 

Jukwaa la mtandaoni la Premier Bet ni jukwaa halali kabisa na lipo kwa mujibu wa sheria. Pamoja na kuwa na  leseni kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Premier Bet inaendeshwa na kampuni ya Entertainment Africa Ltd.

Mapitio ya Premier Bet Tanzania

Kama sehemu ya mapitio ya Premier Bet, tumechambua kila kipengele cha tovuti ya mchezo huu wa kubeti. Hapa chini ni mapitio ya kila kipengele kwenye jukwaa la mtandaoni la Premier Bet. 

Kuingia na Usajili

Mteja yeyote mpya anayetaka kujiunga na Premier Bet Tanzania atahitajika kukamilisha mchakato wa usajili. Ili kukamilisha mchakato, wateja wapya wanatakiwa kuwa na namba ya simu ya mkononi ya Tanzania pamoja na neno salama la siri.

Mara wachezaji wapya wanapojisajili na kuthibitishwa taarifa zao, wanaweza kutumia namba zao za simu na neno la siri ili kuingia kwenye tovuti. 

Promosheni

Mbali na kubeti kupitia Premier Bet, mtoa huduma, yaani bookmaker mara kwa mara hutoa ofa kwa wateja wapya na waliopo. Baadhi ya ofa za Premier Bet mtandaoni zinahusiana kubahatisha matokeo ya michezo kama  kubusti odvile kuongeza fursa za odds, yaanid pamoja na kubeti bila malipo kila wiki.

Hata hivyo, kasino ya Premier Bet pia ina ofa za ziada ambazo wachezaji wanaweza kuzifikia. Ofa hizi ni pamoja na ushindi wa jumla, yaani kushinda jackpot kwenye baadhi ya michezo ya sloti.

Mapitio ya Premier Bet Tanzania

Kubeti Matokeo ya Michezo

Kwa ujumla, Premier Bet Tanzania ina sehemu yenye taarifa za kina za mtoa huduma za kubeti. Kupitia shemu hii, wachezaji wanaweza kuweka dau kwa urahisi kwenye matokeo zaidi ya 20 yaliyopo kwenye masoko ya michezo.

Mbali na michezo maarufu ya kimataifa kama vile mpira wa miguu, wa kikapu na tenisi, pia mtoa huduma ana chaguzi maalumu kwa mpira wa meza na wa mikono. Aidha, mara nyingi mtoa huduma huchapisha nyongeza za urejeshaji pesa na kuongeza fursa za odds ili madau yaliyowekwa yawe na ufanisi.

Esports

Esports ni mashindano ya video games yanayochezwa mtandaoni na mtu mmoja mmoja au kwa timu. Esport ni moja ya masoko ya kubeti yanayokua kwa kasi kwenye eneo la kubeti mtandaoni. Ili kutoa fursakwa wateja wake, Premier Bet Tanzania nayo ina kipengele cha esports.

Wakati mashindano mapya ya esports yanapokaribia, mtoa huduma huchapisha odds kwa ajili ya mashindano haya. Kwa kuongezea, mtoa huduma ana kipengele cha soka mtandao, yaani e-soccer kinachoangazia mashindano ya hivi pinde ya soka mtandao.

Jackpot

Mbali na chaguzi za kawaida za kubashiri matokeo ya michezo, mchezeshaji au mtoa huduma huyu vile vile ana jackpots mbalimbali. Mojawapo ya ofa za jackpot za mtoa huduma ni Super 6. Ili kushinda bonasi ya jackpot, wanaobeti lazima wabashiri kwa usahihi washindi sita kutoka kwenye mechi za soka zilizochaguliwa.

Zaidi ya hayo, wachezaji wanaweza kuingia Jackpot 13 au 15 kwa kuchagua washindi sahihi kutoka kwenye mechi zilizopo.

Ubashiri Mubashara na Live Streaming

Premier Bet Tanzania ina machaguo mengi ya ubashiri mubashara, yaani kubashiri matokeo wakati mchezo umeshaanza. Kwenye Ubashiri Mubashara, yaani Live Betting, wachezaji wanaweza kubeti kwenye matukio mengi ya moja kwa moja kwa saa 24 wiki mzima. Mchezeshaji au Mtoa huduma huendesha odds za moja kwa moja pamoja na masoko kutokana na michezo inavyoendelea.

Aidha, mtoa huduma ana kionyeshi mubashara kinachoonesha taarifa na takwimu za mchezo moja kwa moja ili kuwazesha wanaobeti kufahamu kinachoendelea. Hata hivyo, mapitio ya Premier Bet Tanzania yaligundua kuwa kwa sasa hakuna chaguo la live streaming kwenye tovuti.

Njia za Malipo

Kwenye haya mapitio ya Premier Bet Tanzania, tumeangazia baadhi ya njia za kuweka na kutoa pesa zinazokubaliwa na mtoa huduma. Kufanya malipo, wateja wanaweza kutumia huduma za kutuma pesa kupitia simu ya mkononi. Huduma hizi ni kama vile Airtel Money, M-Pesa, au Tigo Pesa. Vinginevyo, wachezaji wanaweza kutumia vocha za kulipia kabla pamoja na huduma ya simu ya Selcom ili kufanya malipo.

Programu ya Simu, yaani Mobile App

Mtoa huduma huyu wa michezo ya kubashiri anayo programu ya APK inayoweza kupakuliwa kwenye vifaa vya Android. Kwa upande mwingine, tovuti ya kubetia ina toleo la mobile desktop ambalo ni rafiki kwa mtumiaji. Wanaobeti wanaweza kuingia, kujisajili, kufikia masoko ya michezo na odds, na pia kupokea promosheni kupitia jukwaa la kivinjari cha simu.

Kubeti na Premier Bet Tanzania

Mteja yeyote mpya au aliyepo anaweza kushiriki kwa urahisi kubeti na Premier Bet na kuweka dau ndani ya dakika chache. Kabla ya kuweka dau, wachezaji lazima wajisajili kwa mtoa huduma na waingie kwenye akaunti zao. Ifuatayo, wanahitaji kuweka pesa.

Mara tu wachezaji wanapokuwa na pesa kwenye akaunti zao, wanaweza kuelekea kwa mtoa huduma. Kupitia kwa mtoa huduma, hatimae wachezaji wanaweza kuchagua mechi ya kubeti na vile vile kuweka hisa, yaani stake zao kwenye mkeka. Na kupitia masoko ya michezo kwenye tovuti, wateja wanaweza kuweka dau kwenye matokeo yajayo, kama vile washindi wa mashindano na wachezaji mashuhuri.

Vinginevyo, wanaweza kubeti matokeo ya mechi moja moja, mathalani idadi ya chini/juu ya magoli, pointi, mapungufu (handicaps) ya mechi, na ushindi sahihi.

Kwa tovuti ya kasino, wanaobeti wanaweza kutumia pesa zao kuzungusha kwenye michezo ya sloti au kucheza kadi mtandao na kamari zinazochezwa mezani. Kuongezea, wachezaji wanaweza kununua kadi mtandao za kuchanja na kushiriki jackpots za mtandaoni kupitia jukwaa la kasino.

Wakati wa kubeti na mtoa huduma huyu, ni muhimu kufanya maamuzi fikirishi. Mikakati ya msingi ya kubeti, kama vile kuweka jarida la kubeti na kuangalia fomu, inaweza kusaidia kufuatilia madau.

Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara kuhusu Premier Bet Tazania

Ili kuhitimisha mapitio ya Premier Bet Tanzania, tumeangazia baadhi ya maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu mchezeshaji huyu wa mtandaoni.

Jinsi gani ya kuwasiliana na Premier Bet Tanzania?

Timu ya mawasiliano ya Premier Bet inaweza kupatikana kupitia chaneli zifuatazo:
Mitandao ya Kijamii: Facebook
Chat Mubashara (Live Chat): Kuna fomu ya mawasiliano iliyopo kwenye tovuti ya mtoa huduma. Bofya alama ya kiputo cha kijani kinachomaanisha kuongea ili kuanza kuchati moja kwa moja.
Aidha, mtoa huduma anacho Kituo cha Usaidizi cha hali ya juu ambacho kinashughulikia Maswali Yanayoulizwa Mara kwa Mara. 

Unawekaje dau kupitia Premier Bet Tanzania?

Mosi, ili kuweka dau kwa mtoa huduma, wachezaji ni lazima wajisajili na kuweka pesa kwenye akaunti zao. Baada ya hapo, wanaweza kutumia pesa walizoweka ili kubeti kwenye michezo mbalimbali au michezo ya kasino.

Je, Premier Bet Tanzania inatoa huduma ya kubeti kasino?

Ndiyo, jukwaa la kasino la Premier Bet lipo. Wachezaji ambao tayari wana akaunti wanaweza kuzifikia huduma za kasino zitolewazo.

Kwanini Premier Bet haifanyi kazi?

Ukikutana na shida au tatizo lolote la kiufundi kwenye tovuti au app, tafadhali wasiliana na watoa huduma kwa wateja kupitia njia zilizotajwa hapo juu.

18+ | Please play responsibly | Terms and Conditions apply | Commercial Content